• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

KILIMO CHA MCHIKICHI KUSUKUMA UCHUMI MPYA KWA WAKULIMA

Posted on: July 17th, 2025

Na Mwandishi Wetu

Kilimo cha zao la mchikichi katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma kimeanza kuleta mafanikio makubwa kiuchumi kwa wakulima, kufuatia usambazaji wa bure wa mbegu bora aina ya Tenera. Hatua hii imechochea mageuzi makubwa kutoka kilimo cha mazoea kwenda kilimo cha kibiashara, jambo linalotarajiwa kuongeza tija, kipato, na ustawi wa wananchi wa wilaya hiyo.

Akizungumza wakati wa ziara ya waandishi wa habari katika Kijiji cha Kiungwe, Kata ya Kitanga, Kaimu Mkuu wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri  hiyo, Masumbuko Kelemwa, amesema usambazaji wa mbegu hizo umefanyika kwa mujibu wa maelekezo ya serikali bila gharama yoyote kwa wakulima.


“Wakulima wetu wamehamasika kulima zao hili. Kuna mashamba si tu hapa Kiungwe, bali pia katika maeneo kama Rusesa, Bugaga na kata nyingine mbalimbali. Mbegu hizi tunazisambaza bure kabisa. tulianza na hekari 20, baadaye zikazidi kufikia 55, na sasa jumla ya wakulima 2,443 wamepata mbegu hizo na eneo la kilimo limefikia hekta 1,406 huku miche iliyosambazwa ikifikia 175,650,” amesema Kelemwa.


Ameongeza kuwa matarajio ya mavuno ni zaidi ya tani 300,000 kwa mwaka, huku halmashauri ikitarajia kunufaika kupitia ushuru wa mazao yatakayotengenezwa, kwani mazao hayo yanatarajiwa kuuzwaa ndani na nje ya nchi.

_

Mmoja wa wakulima wa zao hilo, Sadoki Mugama, ameishukuru serikali kupitia  Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwaletea mbegu hizo, ambazo huchukua muda mfupi kuanza kuzaa. Ambapo anategemea katika awamu ya kwanza ya mavuno kupata tani moja ya zao hilo, ambayo ni sawa na lita 100,000 za mafuta.


Mwenyekiti wa Serikali ya Kijiji cha Kiungwe, Enock Mugama, amesema kuwa kuna mapinduzi makubwa ya ulimaji wa zao hilo katika kijiji chake kutokana na upatikanaji wa mbegu bora pamoja na mafunzo ya kilimo waliyopewa wakulima bure, jambo ambalo limewafanya wakulima kuwa na matumaini makubwa ya kuboresha maisha yao.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • CPA KAFUKU : WATUMISHI TEMBEENI KIFUA MBELE KWA UTENDAJI KAZI WENU BORA

    July 30, 2025
  • SERIKALI YAKABIDHI SHULE YA SHILINGI 361 KWA KIJIJI CHA ZEZE

    July 24, 2025
  • UGAWAJI WA BURE WA MICHE YA KAHAWA WAWAVUTIA WAKULIMA

    July 22, 2025
  • KILIMO CHA MCHIKICHI KUSUKUMA UCHUMI MPYA KWA WAKULIMA

    July 17, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.