• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

MSAADA WA JKT WAOKOA ZAIDI YA MILIONI 13 KWA SHULE YA MGOMBE

Posted on: August 18th, 2025

Na Mwandishi Wetu 

Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) kupitia Kikosi cha 825 Mtabila leo Jumatatu kimekabidhi madawati 250 na meza sita vyenye thamani ya shilingi 7,278,400 kwa Shule ya Msingi Mgombe, wilayani Kasulu. Hatua hiyo imepunguza changamoto ya miundombinu ya kufundishia na kujifunzia shuleni hapo.

Aidha, kikosi hicho kimekarabati madawati 45 na hivyo kumaliza kabisa upungufu wa samani hizo, sambamba na kuwasaidia walimu saba kufundisha wanafunzi kwa lengo la kuboresha kiwango cha elimu.

Akizungumza katika makabidhiano hayo, Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Mhe. Kanali Isaac Mwakisu amemshukuru Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa, Meja Jenerali Rajabu Mabele, kwa kuruhusu kambi hiyo kutekeleza jukumu hilo, jambo alilosema limeokoa zaidi ya shilingi milioni 13.

“Nimeambiwa thamani ya dawati moja ni shilingi 70,000, hivyo mmeokoa zaidi ya shilingi milioni 13 kama Mtabila wasingesaidia. Nawasihi jamii ya hapa muendelee kushirikiana na majirani zenu, mkikaa hapa mnakaa kama Watanzania. Shirikianeni ili kukuza ustawi wa nchi yetu,” amesema Kanali Mwakisu.

Aidha, amekiomba kikosi hicho, ambacho kina mikakati ya kuanzisha chuo cha ufundi wilayani humo, kitoe maombi ya eneo katika Kijiji cha Mgombe ili kutekeleza mpango huo, akisisitiza kuwa chuo hicho kitakuwa na tija katika kufundisha fani mbalimbali.

Kwa upande wake, Kamanda wa Kikosi hicho, Luteni Kanali Patrick Ndwenya, amewahimiza wananchi wanaoishi vijiji vinavyozunguka kambi hiyo wasisite kuwasiliana nao wanapokumbana na changamoto mbalimbali, ili taratibu zifuatwe na msaada upatikane kwa wakati.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, CPA Francis Kafuku, ameishukuru kambi hiyo kwa msaada huo, akibainisha kuwa ofisi yake itahamasisha vijiji vingine kuiga mfano wa Shule ya Msingi Mgombe kwa kuwa wanufaika wakuu ni watoto.


Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MPANGO WA UWAWA WAIBUA MATUMAINI MAPYA KATIKA SEKTA YA ELIMU KASULU

    August 20, 2025
  • MSAADA WA JKT WAOKOA ZAIDI YA MILIONI 13 KWA SHULE YA MGOMBE

    August 18, 2025
  • TANZANIA NA BURUNDI ZAANZA RASMI UJENZI WA RELI YA KISASA YA UVINZA-MUSONGATI

    August 16, 2025
  • WATUMISHI HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU WAMPONGEZA MKURUGENZI KAFUKU KWA KUSIKILIZA KERO ZAO HADI NGAZI YA KATA

    August 14, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.