• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

WAZIRI MKUCHIKA AONGEA NA WATUMISHI WA UMMA KASULU

Posted on: September 24th, 2018

Watumishi wa Halmashauri ya Mji na Wilaya Kasulu wakimsikiliza  Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapteni (Mstaafu), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) (hayupo pichani) alipokutana na kuzungumza nao  leo katika Ukumbi wa Chuo cha ualimu Kasulu.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapteni (Mstaafu), Mhe. George H. Mkuchika (Mb)(Mwenye suti nyeusi) akifafanua jambo wakati alipokutana na kuongea na watumishi wilayani Kasulu.

Na. Andrew Mlama-Kasulu.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Kapteni (Mstaafu), Mhe. George H. Mkuchika (Mb) amekutana na kuongea na watumishi wa Umma toka Idara na Vitengo  mbalimbali katika  halmashauri ya Mji na Wilaya Kasulu.

Mkuchika amekutana na kuongea na watumishi hao leo Tarehe 24.09.2018 katika Ukumbi wa chuo cha Ualimu Kasulu, ambapo amewapongeza watumishi hao kwa kazi nzuri wanazozifanya kisha kusikiliza kero zao na kutoa ushauri wa namna bora ya kuzitatua.

Amesema utumishi wa umma ni pamoja na matumizi bora ya taaluma, nidhamu, kuzingatia kanuni za utumishi ili kuwa mfano wa kuigwa katika jamii. Amewashauri watumishi washirikiane katika kufanya kazi na kuongeza nguvu kukusanya mapato ili serikali iweze kuendelea kutekeleza miradi ya maendeleo.

Amefafanua  kuhusu zoezi la uhakiki wa vyeti, ambapo amesema kuwa suala hilo lilizingatia Sheria na kanuni za kiutumishi. Kwa wale walioondolewa na kuthibitika  hawana dosari za kiutumishi walirejeshwa kazini na kulipwa stahiki zao zote.

“Waliodanganya  kiwango cha elimu, kugushi vyeti na walioajiriwa baada ya tarehe 20.Mei 2004 wakiwa hawana sifa ya ufaulu ya Mtihani wa Kidato cha nne, waliondolewa kazini  kwa kuwa walijipatia ajira kinyume na utaratibu wa Serikali”amesema Mkuchika.

Waziri Mkuchika amewataka Wakurugenzi kutozuia barua za maombi ya uhamisho wa watumishi waliotimiza vigezo, bali watoe maoni yao kisha waruhusu barua zifike kwa aliyeandikiwa. Aidha amewataka Wakurugenzi watumie sababu za kibinaadamu kuruhusu uhamisho wa mtumishi endapo sababu za msingi zitathibitika.

Ametoa Rai kwa watumishi walioajiriwa Kigoma kuamini kwamba, wameajiriwa ili kuwezesha Wananchi kupata huduma na isiwe ni sehemu ya kupatia ajira kisha kuwaacha wananchi bila huduma.

Wakati huo huo Waziri Mkuchika, amewaasa watumishi wanaohusika na ukusanyaji mapato,jeshi la  Polisi, Wauguzii na Sehemu nyingine zinazotoa huduma kwa Umma, waache na kuepuka vitendo vya Rushwa. Amesisitiza wafanye kazi kwa uadilifu ili kutoa huduma yenye usawa kwa wananchi wote.

Waziri Mkuchika amehitimisha ziara yake katika Halmashauri ya Wilaya ya  Kasulu kwa kutembelea Kata ya Kitagata ambapo amezungumza na walengwa wa TASAF na kukagua shughuli za maendeleo pamoja na mafanikio yaliyofikiwa kutokana na mradi huo.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • PAMBA KUINUA UCHUMI WA WAKULIMA

    May 08, 2025
  • WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WAHASWA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.