• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

WATUMISHI AJIRA MPYA KADA YA WATENDAJI WA VIJIJI WAPEWA MAFUNZO ELEKEZI KASULU.

Posted on: October 29th, 2018

Afisa Tawala wa Halmashauri ya wilaya ya Kasulu ndg. Nicholaus Elihaki akiwasilisha mada  wakati wa utoaji wa mafunzo kwa watumishi waajira mpya kada ya watendaji wa vijiji yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya  Kasulu.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kasulu, Ndg. Nimrod Kiporoza akifafanua jambo wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya watumishi wa ajira mpya kada ya watendaji yaliyofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Kasulu. kushoto kwake ni Afisa Utumishi wilaya ya Kasulu ndg. Charles Millinga pamoja na Afisa Tawala (W) Nicholaus Elihaki

Mratibu wa TASAF Halamshauri ya wilaya Kasulu, Almachius Njungani akiwasilisha mada kwenye mafunzo elekezi kwa watumishi wapya kada ya watendaji wa vijiji yaliyofanyika wilayani hapa.

Na. Andrew Mlama-Kasulu.

Watumishi wa  ajira mpya kada ya watendaji wa vijiji  walioajiriwa kati ya mwaka 2015 hadi  2018, wamepatiwa mafunzo elekezi yatakayowasaidia katika kuboresha utendaji wao wa kazi  ili kuhakikisha ufanisi katika utekelezaji wa majukumu  katika maeneo yao ya utendaji kazi  wilayani hapa.

Akifungua mafunzo hayo yaliyofanyika leo tarehe 29/10/2018 katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya kasulu,  Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kasulu ndg. Nimrod Kiporoza  amewataka watendaji hao kuzingatia maelekezo yatakayotolewa ili wakayatumie katika kuboresha utendaji kazi wao kwa kuzingatia sheria kanuni na maadili ya kiutumushi.

Amesisitiza kuwa, mafunzo hayo yatumike kukumbushana majukumu ya utendaji yanayohusu maeneo mbalimbali ya utendaji kazi .Aidha amewataka wataalam wa Idara na Vitengo vingine wasaidie kutoa maelekezo na ujuzi kwa watendaji hao utakaosaidia kupanua uelewa wa  mambo mengi zaidi ya utendaji kazi.

“Jifunzeni vizuri ili mjue Sheria na Kanuni zinazowaongoza katika utendaji kazi wenu ili msiyumbishwe pale mnaposimamia utekelezaji wa kazi. Ikumbukwe watendaji ndio wasimamizi wa utekelezaji wa kazi na shughuli nyinginezo za maendeleo vijijini”amesema Kiporoza.

Akiwasilisha mada, Afisa Tawala wa Halmashauri ya wilaya ya Kasulu ndg. Nicholaus Elihaki amefafanua kuwa, utumishi wa Umma unategemea nidhamu kubwa kwa watumishi ili kuepuka migogoro na muajiri itakayopelekea kuchukuliwa hatua za kinidhamu. Amesema watumishi wanapaswa kufikia malengo ya kinidhamu ili kudumisha utumishi wenye weledi. Amesisitiza watumishi waepuke makosa makubwa na madogo ya kuitumishi ili kujiepusha na migogoro dhidi ya muajiri na jamii wanayoihudumia.

‘’Watumishi wa tuhakikishe tunazingatia kanuni za utendaji katika utumishi wa umma, ikiwemo kuzingatia masaa ya kazi, mahudhurio sahihi, kuzingatia kanuni na miongozo ya kazi katika jamii tunazoishi na mazingira tunayofanyia kazi. suala la upandishwaji vyeo, kuthibitishwa kazini pamoja na huduma nyingine za kiutumishi ni jukumu la muajiri kuendana na miongozo iliyowekwa” amehitimisha Afisa Tawala.

Afisa utumishi wa halmashauri ya wilaya ya Kasulu, ndg. Charles Millinga, amewasilisha mada kwa kuwafafanulia watumishi hao kuhusu haki na wajibu wa mwajiri pamoja na mtumishi, namna bora ya mawasiliano katika ofisi za Umma,taratibu za mafunzo na kujiendeleza kitaaluma, ujazaji wa OPRAS, kanuni bora za utendaji kazi na nidhamu kwa watumishi wa Umma. 

Wakuu wa idara na vitengo vya manunuzi na ugavi, fedha, kilimo, utumishi na utawala, sheria, uchaguzi, ardhi na maliasili, maendeleo ya jamii pamoja na TASAF walipata fursa ya kuwasilisha mada zao na kutoa maelekezo ya kiutendaji kwa watumishi hao ili kuwajengea uwezo, uelewa na ufahamu wa utekelezaji majukumu yao kwa mujibu wa sheria na miongozo ya seriakali.

Kwa upande wao, watendaji  wameonyesha kufurahishwa na mafunzo hayo na kuiomba Idara ya utumishi na utawala na halmashauri kwa ujumla, kutoa mafunzo hayo mara kwa mara ili kuwajengea weledi na uelewa wa masuala mbalimbali ya utendaji kazi. “Mafunzo haya yamepelekea kujijengea uwezo katika utendaji kazi kwa kutupa  ufahamu wa kutatua changamoto mbalimbali. Aidha yametuwezesha kufahamu sheria kanuni na taratibu za kazi ambazo hapo awali hatukuwa na ufahamu nazo” alihitimisha Emiliano Fabiano,  afisa Mtendaji wa kijiji cha Mgombe kata ya Nyakitonto wilayani hapa.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • PAMBA KUINUA UCHUMI WA WAKULIMA

    May 08, 2025
  • WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WAHASWA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.