• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

WALIMU WA SHULE YA MSINGI BOMBWE WAPEWA MOTISHA

Posted on: December 20th, 2022


Katika hali inayoonesha kufurahishwa na matokeo ya wanafunzi wa Shule ya Msingi Bombwe katika mtihani wa kuhitimu darasa la saba uliofanyika Novemba mwaka huu, afisaelimu msingi wa halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Elestina Chanafi ametoa motisha ya shilingi laki moja kwa walimu wa shule hiyo.

Tukio hilo limetokea shuleni hapo mapema wiki hii wakati wa kikao cha wazazi na walimu kilichohudhuriwa na afisaelimu wa halmashauri ya Wilaya ya Kasulu na maofisa wengine.

Akisoma taarifa ya shule hiyo, mwalimu mkuu wa shule ya msingi Bombwe Neberth Lilabhabha amebainisha kuwa,  shule ya msingi Bombwe imekuwa ya kwanza kwenye matokeo ya mtihani wa kuhitimu darasa la saba kati ya shule 77 za halmashauri ya Wilaya ya Kasulu zilizokuwa na watahiniwa wa mtihani huo.

Amesema kuwa shule hiyo yenye walimu 6 na wanafunzi 886, ilikuwa na watahiniwa 57 wa darasa hilo kati yao 21 ni wasichana na 36 ni wavulana na wote wamefaulu mtihani huo.

"Wanafunzi wote wamechaguliwa kwenda shule za Sekondari tumefaulisha kwa asilimia mia moja," alisema mwalimu mkuu alipokuwa akisoma taarifa hiyo.

Matokeo hayo ambayo hayajawahi kufikiwa na shule hiyo tangu ilipoanzishwa takribani miaka 39 iliyopita, yalimwinua afisaelimu wa halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Bi, Elestina Chanafi na kuwaambia kuwa, atatoa motisha ya shilingi laki moja kwa walimu wa shule hiyo.

"Natoa pesa hizo mfukoni mwangu iwe motisha kwa kazi nzuri mliyoifanya, mtaamua wenyewe kama mtanunua mbuzi mjipongeze ama vyovyote ", alisema Chanafi na kuwapongeza pia wazazi na viongozi wa kijiji na wa kata hiyo.

"Kutokana na mafanikio haya nimewapenda watu wa shule hii hata kabla ya kuwajua na nikaona leo nije tuonane", aliongeza Chanafi wakati wa hotuba yake.

Kikao hicho kilichohudhuriwa pia na diwani wa kata ya Buhoro Mathias Sunzu, kilikuwa na mafanikio makubwa hasa baada ya wajumbe wa kikao hicho kukubali kuyaendeleza mambo mbalimbali yaliyochagiza kupatikana kwa mafanikio hayo.

Makubaliano ya kikao hicho ni pamoja na wazazi kuhudhuria katika vikao pindi wanapohitajika, kukabiliana utoro wa wanafunzi, kuwepo kwa kambi ya kujiandaa na mitihani, kuchangia chakula cha wanafunzi, kuchangia malipo ya walimu wa kujitolea sanjali na kufuatilia maendeleo ya watoto wao wawapo shuleni.



Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MPANGO WA UWAWA WAIBUA MATUMAINI MAPYA KATIKA SEKTA YA ELIMU KASULU

    August 20, 2025
  • MSAADA WA JKT WAOKOA ZAIDI YA MILIONI 13 KWA SHULE YA MGOMBE

    August 18, 2025
  • TANZANIA NA BURUNDI ZAANZA RASMI UJENZI WA RELI YA KISASA YA UVINZA-MUSONGATI

    August 16, 2025
  • WATUMISHI HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU WAMPONGEZA MKURUGENZI KAFUKU KWA KUSIKILIZA KERO ZAO HADI NGAZI YA KATA

    August 14, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.