• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

MRADI WA BUHOMA UNAFUNGUA JAMII AKILI NA UWEZO KATIKA KUJILETEA MAENDELEO

Posted on: February 19th, 2024

Na Mwandishi Wetu

Shirika la World Vision kupitia mradi wa Buhoma kwa kutumia mtindo wa Mtazamo Chanya limekuwa linatoa mafunzo kwa jamii  ili kuiwezesha  kufunguka kiakili na kiuwezo  iweze  kuona  fursa mbalimbali zinazowazunguka na kuzifanyia kazi kwa lengo la kuwaletea maendeleo.

 Hayo yamebainishwa wilayani Kasulu mkoani Kigoma hivi karibuni na Mwezeshaji wa Mradi huo, Zablon Choma kwenye kikao cha kufanya tathimini kwa wanufaika wa mradi ni jinsi gani mafunzo waliyopata yameweza kuinufaisha jamii inayowazunguka.

 Amesema mradi huo unafanya kazi kwenye Tarafa ya Makere yenye kata nane na vijiji 10 kwa kushirikiana na serikali ili kutatua changamoto zinazoikabili jamii katika eneo hilo.

“Mwaka jana kwa kushirikiana na viongozi wa serikali tulipata wawakilishi 12 kutoka vijiji 10 na kuwajengea uwezo na baada ya kuwafundisha wakarudi katika vijiji vyao kwenda kufanya mambo mbalimbali katika sekta ya kilimo, ufugaji na biashara,” amebainisha.

Mmoja wa wanufaika wa mradi huo  Evaristo Milagrokasase amesema kupitia mafunzo hayo amepata uelewa kuwa mtu akitaka kufanikiwa si lazima aende mbali bali  awe na uwezo wa kuzitumia kikamilifu fursa zinazomzunguka katika eneo lake la karibu.

“Awali nilikuwa nalima kilimo cha kawaida lakini mwaka uliopita nilipata kujua Pamba ni dhahabu nyeupe hivyo mwaka huu nina mpango wa kulima heka mbili na mahindi tayari nimelima heka saba, na kupata pongezi nyingi kwa namna ninavyoendesha kilimo changu,” amebainisha.

Mnufaika mwingine Emelisiana Manyurane  amebainisha kuwa kupitia shughuli za ufugaji alizoanza kuzifanya  baada ya mafunzo amefanikiwa kusomesha watoto wake wanne na mjukuu mmoja, kujenga nyumba pamoja na kununua kiwanja chenye thamani ya shilingi milioni 1.2.

Naye Afisa Kilimo wa Kata ya Kitagata, Eliud Mteze amesema kuwa jukumu lake katika mradi huo ni kuwaelimisha wakulima kuachana na kilimo cha mazoea na badala yake wahamie katika mtindo ule wa biashara.

“Kwa kutambua hilo nimeanza na vikundi vinavyojihusisha na shughuli hizi kwa kutoa huduma za ushauri bure na pale ninapokutana na mapungufu najitahidi kuwaelimisha ili wafanye kilimo pamoja na ufugaji wenye tija,” amesema.

Akifunga kikao hicho Afisa Maendeleo ya Jamii, Jotham Daniel amesema ufuatiliaji wa yale yote yaliyozungumzwa utaanza  kufanyika hivi karibunii ili kujiridhisha  uhalisia wake kama ni kweli.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • PAMBA KUINUA UCHUMI WA WAKULIMA

    May 08, 2025
  • WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WAHASWA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.