• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

MAFUNZO YA MAKARANI WA SENSA KASULU YAHAMIA VIJIJINI

Posted on: August 11th, 2022

Makarani wa sensa ya watu na makazi wa halmashauri ya Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma waliokuwa wakifanyia mafunzo yao kwenye chuo cha ualimu Kasulu, wamehamishia mafunzo hayo katika vijiji vya Makere, Nyakitonto, Kasangezi na Rungwe mpya.


Mabadiliko ya mahali pa kufanyia mafunzo hayo yanatokana na takwa la mwongozo wa sensa ya watu na makazi wa mwaka 2022 kuhusu kufanyika kwa mazoezi ya kudodosa ambapo kwa makarani wa halmashauri za vijijini wanatakiwa kufanya mazoezi hayo kwa kuhoji kaya zilizo katika maeneo ya vijijini kama ilivyo kwa makarani wa halmashauri za mijini wanaotakiwa kufanyia mazoezi hayo kwa kuhoji kaya za mjini.


Akizungumza muda mfupi kabla ya makarani hao kuanza safari ya kwenda vijijini, mkuu wa Wilaya ya Kasulu Kanali Isack Mwakisu aliyefanya ziara ya kukagua maendeleo ya mafunzo hayo, amewaasa makarani hao kuvitunza vishikwambi walivyokabidhiwa kwa ajili ya kazi hiyo na kujiepusha na ulevi muda wote watakapokuwa kwenye kazi hiyo.


"Kavitunzeni vishikwambi hivyo kama mboni za macho yenu maana hivyo ndio vitendea kazi vyenu, na mimi nawaombea kwa mungu mtakapokuwa huko, pepo la ulevi lishindwe na mkaifanye kazi hiyo kwa mafanikio makubwa", alisema.


Kufuatia mabadiliko hayo, zaidi ya makarani 1300 waliokuwa kwenye mafunzo hayo kituo cha chuo cha Ualimu Kasulu, wameondoka kuelekea vijijini wakiambatana na wakufunzi wao.


Watakapokuwa huko, sambamba na kufanya mazoezi kwa vitendo, makarani hao pia watafundishwa jinsi ya kujaza dodoso la jamii na dodoso la majengo madodoso ambayo yamepangwa kufundishwa wakati wa mazoezi hayo.


Mafunzo hayo yaliyoanza Julai 31, yanatarajiwa kufikia kikomo Agosti 19 siku chache kabla ya kuanza kwa zoezi la kuhesabu watu.

Pichani makarani wakimsikiliza mkuu wa Wilaya ya Kasulu alipofika kuzungumza nao.



Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • PAMBA KUINUA UCHUMI WA WAKULIMA

    May 08, 2025
  • WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WAHASWA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.