• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

KASULU DC YAKABIDHI GARI LA SHILINGI MILIONI160 KWA SHULE YA HOPE

Posted on: October 18th, 2025

Na Mwandishi Wetu 

Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma leo Jumamosi Oktoba 18, 2025, imefanya tukio la kihistoria kwa kukabidhi basi jipya la kisasa lenye thamani ya Shilingi milioni 160 kwa shule ya Hope Pre and Primary, yenye mchepuo wa Kiingereza, kwa ajili ya kubebea wanafunzi. Basi hilo limenunuliwa kupitia mapato ya ndani ya halmashauri.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Mhe. Kanali Isaac Mwakisu, amempongeza Mkurugenzi kwa jitihada zake za kuboresha miundombinu ya shule, ikiwemo ujenzi wa bweni na ununuzi wa gari jipya. Amesema hatua hizo zitavutia wazazi kutoka sehemu mbalimbali kuwaleta watoto wao shuleni hapo.

“Shule hii inatakiwa kuwa kubwa na ya mfano kwani ndiyo ya kwanza mkoani kufundisha mchepuo wa Kiingereza. Namwelekeza Mwalimu Mkuu kuhakikisha miundombinu iliyopo inatunzwa vizuri, na yule atakayepatiwa dhamana ya kuendesha gari hili ahakikishe anabeba wanafunzi kwa usalama,” amesema Kanali Mwakisu.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo, CPA Francis Kafuku, amemshukuru Rais kwa kuridhia matumizi ya fedha za mapato ya ndani ya halmashauri kuboresha miundombinu ya shule hiyo, ikijumuisha bweni na ununuzi wa gari, hatua ambayo itasaidia ubora wa ujifunzaji na ufundishaji.

“Mahitaji yote yanatokana na mapendekezo ya madiwani, ambayo halmashauri inampelekea Mkuu wa Wilaya kubariki. Tunamshukuru Mkuu wa Wilaya kwa kubariki mambo haya, kwani angeweza kukataa fedha hizo ziende kwa miradi mingine,” amesema CPA Kafuku.

Kwa upande wake, Afisa Elimu Awali naMsingi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, Elestina Chanafi, amesema kuwa kutokana na muitikio mkubwa wa wazazi kuleta watoto shuleni hapo, kulikuwa na changamoto ya usafiri.Hivyo  basi  hilo jipya litasaidia kupunguza adha hiyo kwa wanafunzi.


Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • KASULU DC YAKABIDHI GARI LA SHILINGI MILIONI160 KWA SHULE YA HOPE

    October 18, 2025
  • MAAFISA UGANI WATAKIWA KUHAMASISHA USAJILI WA WAKULIMA KWENYE MFUMO WA RUZUKU

    October 08, 2025
  • SERIKALI YAENDELEA KUWAUNGA MKONO WAKULIMA WA PAMBA KASULU

    October 07, 2025
  • LALJI FOUNDATION YATOA MADAWATI 100 KUSAIDIA SHULE TATU

    October 04, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.