• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

KAMCHAPE HAIKUBALIKI TUSHIRIKIANE KUITOKOMEZA

Posted on: April 5th, 2024

Na Mwandishi Wetu

Wananchi wilayani Kasulu mkoani Kigoma wametakiwa kuunganisha nguvu kuwapinga wapiga ramli chonganishi maarufu kama Kamchape   kwakuwa wanadhalilisha watu kupitia vitendo wanavyofanya.

Hayo yamebainishwa jana na Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Mhe. Kanali Michael Ngayalina alipofuturisha makundi mbalimbali ya watu katika wilaya hiyo.

Amesema wananchi wanapaswa kuhamka na kupambana na kundi hilo la kitapeli linaloibia watu kupitia mazingaombwe wanayofanya na kuwatuhumu  watu kuwa ni wachawi na kujenga chuki katika jamii.

“Viongozi wa dini mliopo hapa sauti yenu itangulie mbele kwakuwa huwa mnaongoza jamii kwenye kutafsiri maandiko jukwaa lenu naliona lina nguvu hivyo tunaomba mtusaidie katika hili,” amesema.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kasulu, Mbelwa Chidebwe amesema wamejipanga kupita maeneo mbalimbali ya wilaya kukemea vitendo hivyo vya kihuni na kitapeli.

“Niwaombe wote tushikamane katika hili katika mwezi huu  Mtukufu   tumuombe Mungu kupitia dua zetu hatuepushe na hili kwakuwa ni shirki na katika imani yetu sisi Waislamu shirki ni dhambi ,” amesema.

Kwa upande wake Sheikh Mkuu wa Wilaya Hiyo,Masoud Kukoba amefarijika kuona Futari hiyo imejumuisha watu kutoka nyanja tofauti  kukaa pamoja kwa upendo na kuzitaka halmashauri zingine kuiga mfano huo.  

Naye Mwenyekiti wa Makanisa ya Kipentekoste (CPCT) Wilaya ya Kasulu, Mchungaji Wilbert Muhoza amebainisha kuwa  Mungu aliyetuumba kwa mfano wake huwa anafurahi kuona watu wa imani tofauti wanapokaa kwa pamoja na kusikilizana.

Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, Emmanuel Ladislaus amesema kuwa   dhamira ya Mkuu wa Wilaya kuandaa Futari hiyo ni kutaka kuchota sawabu zinazotokana na kufuturisha watu waliofunga.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Kasulu,Vumilia Simbeye  amesema tukio hilo limefanikiwa kutokana na serikali kuendelea kudumisha  amani na utulivu miongoni mwa watu.

Katika hatua nyingine Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, Mhe. Eliya Kagoma amebainisha kuwa Upendo na umoja unaoitambulisha nchi yetu katika anga la kimataifa umeoneshwa kwa vitendo kwa waudhuriaji wa tukio hilo.



Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • KUU KASULU YAKAGUA MIRADI YA MWENGE

    June 13, 2025
  • MATUMIZI YA ZANA ZA UFUNDISHAJI YATAJWA KUONGEZA UFANISI SHULENI

    June 11, 2025
  • WALIMU SHULE YA MSINGI KISUMA WATOA SHUKRANI KWA WADAU WALIOCHANGIA SARE NA VIFAA KWA WANAFUNZI

    June 05, 2025
  • MAFUNZO YA SIKU TATU YA KKK KWA WALIMU WA DARASA LA KWANZA NA LA PILI YAFIKIA TAMATI KASULU

    June 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.