• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU YATOA MKOPO WA SHILINGI MILIONI 40 KWA VIJANA.

Posted on: April 10th, 2023

Na Mwandishi Wetu


Kufuatia maelekezo ya serikali kuzitaka mamlaka za halmashauri nchini kutenga asilimia kumi ya fedha zitokanazo na mapato ya ndani kwa ajili ya mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, halmashauri ya Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma imeendelea kuwa kinara wa kutekeleza agizo hilo.


Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi pikipiki 15 zenye thamani ya shilingi milioni 40 kwa kikundi cha vijana cha "Twaweza" kutoka katika kata ya Makere, mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Eliyah Kagoma amewataka vijana waliopata mkopo huo  kutumia nguvu na akili katika kazi yao.


Amewaambia kuwa pikipiki hizo hawajapewa bure hivyo zinatakiwa zitumike kama mtaji utakaowawezesha kupata pesa ili kurejesha gharama zilizotumika kununua pikipiki hizo na kujijengea imani kwa serikali.


Aidha amewataka vijana hao kuepuka kuzitumia pikipiki hizo katika matumizi maovu yakiwemo ya kuchepusha mapato ya halmashauri na kusafirisha wahalifu na badala yake waisaidie halmashauri kwa kutoa taarifa ya uchepushaji wa mapato kwa kuzingatia kuwa kutokana na kupewa mkopo huo, na wao sasa ni sehemu ya halmashauri.


"Mjue kuwa pesa za mkopo wa kununulia pikipiki hizo zimetokana na makusanyo ya ndani hivyo mkiona watumishi wa halmashauri wanakuja kukusanya ushuru, tozo na mapato mbalimbali toeni ushirikiano, huko ndiko zilipotoka pesa zilizonunua pikipiki hizo" amewaambia.


Akitoa maelezo kuhusu mkopo huo, Afisa Maendeleo ya jamii wa halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Victoria Makyao amesema kuwa, katika kipindi cha mwaka wa fedha wa 2022 na 2023, halmashauri ya Wilaya ya Kasulu imetoa mikopo yenye thamani ya shilingi 208,000,000.


Amefafanua kuwa kati ya fedha hizo, shilingi 95,000,000 zimetokana na makusanyo ya mapato ya ndani huku shilingi 113,000,000 zikiwa zimetokana na marejesho ya mikopo hiyo.


Makyao ameongeza pia kuwa kupitia pesa hizo, jumla ya vikundi 24 vimenufaika na kuvitaja vikundi hivyo pamoja na mikopo waliopata kuwa ni shilingi 87,000 zilitolewa kwa vikundi 13  vya wanawake, shilingi 95,000,000 zilitolewa kwa vikundi 8 vya vijana huku shilingi 26,000,000 zikienda kwa vikundi 3 vya watu wenye ulemavu. 


Kuhusu hali ya marejesho, taarifa ya Makyao imeeleza kuwa, hadi kufikia Machi 30 mwaka huu, jumla ya shilingi 326,252,492 zimerejeshwa.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • PAMBA KUINUA UCHUMI WA WAKULIMA

    May 08, 2025
  • WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WAHASWA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.