• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

DCC HALMASHAURI YA KASULU WAPITISHA MPANGO NA BAJETI 2019/2020.

Posted on: February 25th, 2019

Mkurugenzi wa halmashauri ya Kasulu Mhandisi. Godfrey Kasekenya, akitoa ufafanuzi  kwa wajumbe(hawapo pichani) kabla ya kuanza  kikao cha Kamati ya Ushauri ya Maendeleo Wilaya kujadili Mpango na Bajeti kwa mwaka wa Fedha 2019/2020 kilichofanyika leo tarehe 25/2/2019 kwenye ukumbi wa Halmashauri.

Mkuu wa Wilaya ya Kasulu  Kanali. Simon Anange akisisitiza jambo, wakati akifungua  kikao  cha Kamati ya Ushauri ya Maendeleo  wilaya, kujadili Mapitio ya Mpango na Bajeti kwa mwaka wa Fedha 2019/2020.

Mwakilishi  toka Shirika la  Mpango wa Chakula Duniani (WFP) wilayani Kasulu Ndg. Michael Bisama, akichangia hoja. Mashirika mbalimbali pamoja na Taasisi zisizo za Kiserikali ni  wadau  Muhimu  katika kuchangia Bajeti ya Halmashauri ya wilaya ya Kasulu.

Na.Andrew Ginnethon.

Kikao cha Kamati ya ushauri ya Maendeleo Halmashauri ya wilaya ya Kasulu, kimepitia Mapitio ya Mpango na Bajeti kwa Mwaka 2017/2018,2018/2019 na Makisio na  kupitisha Mpango na Bajeti kwa Mwaka wa fedha 2019/2020 wilayani hapa.

Akifungua Kikao hicho,  Mkuu wa wilaya ya Kasulu Kanali.  Simon Anange amewataka wajumbe kutoa ushauri na mawazo yenye tija kuhusu Mpango na Bajeti hiyo kwa lengo la kuboresha huduma kwa Jamii.

Aidha ameyataka Mashirika yanayotoa huduma kwa wakimbizi waliopo wilayani hapa, kujielekeza  katika  kuisaidia Jamii ya wakazi wenyeji ambao wanaathiriwa kiasi kikubwa na uwepo wa Wakimbizi hao.

“Mashirika mengi yameshindwa kuisaidia Jamii  kwa kutoa misaada yenye tija kwa wananchi  bali imekuwa ikitolewa misaada isiyo endelevu ambayo manufaa ya muda mrefu kwa wakazi wanaozunguuka maeneo wanayoishi wakimbizi” amesema Anange.

Akizungumza na wadau wa Mkutano huo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kasulu Mhandisi Godfrey Kasekenya, amesema uwepo wa wadau wa maendeleo ni muhimu ili kufahamu watachangia kiasi gani katika Bajeti hiyo.

Ameshauri kuwa, Mashirika mbalimbali yanapotoa misaada ni lazima yawasiliane na Halmashauri ili kuepuka kutekeleza mpango mmoja kwa pamoja na badala yake Halmashauri ijielekeze kwenye utekelezaji mipango mingine.

Akiwasilisha Makisio ya  Mpango na Bajeti kwa Mwaka 2019/2020, Afisa Mipango Takwimu na Ufuatiliaji  wa Wilaya Ndg. Jackob Kilatu, amesema halmashauri imekisia kutumia zaidi ya Shilingi Bil 48.2 katika kutekeleza Miradi mbalimbali na uendeshaji wa Halmashauri.

Ndg. Mbela Abdallah, Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi wilaya,  amepongeza maandalizi mazuri na mchakato mzima uliofanywa na wataalam kwa kushirkikana na Mkurugeni hali iliyopelekea Mpango na Bajeti hiyo kufikia hatua iliyopo.

Akishangia Mapendekezo ya Mpango na Bajeti,  katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo wilaya Ndg.Rajabu Bujoro  ameshauri kwenye Bajeti ijayo, uwepo mkakati mkubwa wa utunzaji wa Mazingira pamoja na vyanzo vya Maji.

Wajumbe walihitimisha kikao kwa kauli moja ya kuukubali na kuupitisha mpangona  huo kwa lengo la Maendeleo ya wilaya ya Kasulu na Taifa kwa ujumla katika kuhakikisha huduma inawafikia wananchi katika ubora.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • PAMBA KUINUA UCHUMI WA WAKULIMA

    May 08, 2025
  • WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WAHASWA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.