• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

WALIMU WATAKIWA KUTIA JUHUDI KUFAHAMU MIFUMO YA KIDIGITALI

Posted on: February 23rd, 2024


Na Mwandishi Wetu.

Walimu katika Halmashauri  ya Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma wametakiwa kutia juhudi kwenye kuielewa mifumo mbalimbali ya kidigitali ya serikali wanapotekeleza majukumu yao ya kila siku kwenye vituo vyao vya kazi.

  Afisa Elimu Mkoa wa Kigoma, Paulina Ndigeza  ameyabainisha hayo wilayani humo  jana kwenye hafla ya Siku Maalumu ya Elimu kwa Mwaka 2024 iliyojikita kutoa tuzo kwa walimu na shule mbalimbali zilizofanya vizuri katika mitihani mbalimbali ya kitaifa ya upimaji kwa mwaka 2023.

“Kila mmoja lazima ajifunze mifumo kwakuwa mambo ya kiutumishi kama OPRAS yapo kwenye mfumo ndio maana watumishi wote tunatakiwa kujisajili, kwahiyo vigezo vyote vya utendaji kazi vilivyokuwa vinatumia karatasi sasa hivi mambo hayo hakuna na huo ni mfumo wa nchi nzima,” amesema.

Pia, ameshauri ushirikishwaji wa jamii katika suala la kudhibiti utoro ili kuongeza kiwango cha ufaulu.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Emmanuel Ladislaus amesema kuwa kikao hicho kimefanyika ili kufanya tathimini ya kina itakayofanya maboresho kutoka mahali walipokuwa na kusonga mbele kwenye suala la taaluma.

“Katika halmshauri yetu tunajivunia kufanya vizuri na hilo tumelifanya kwa vitendo pamoja na jiografia yetu amabayo huwezi kuichora kwa urahisi lakini tumeweza kutumia rasilimali ndogo tulizokuwa nazo kufanya mambo makubwa kwenye suala la taaluma kwa mwaka uliopita.

Afisa Elimu Sekondari Taaluma, Mussa Kanyoe  akitoa taarifa ya sekta ya elimu kwa mwaka uliopita amebainisha kuwa kumekuwa na ongezeko la uandikishaji wa wanafunzi wa elimu ya awali kutoka 97% mwaka 2022 kufikia 105% kwa mwaka 2023.

“Kwa Darasa la Kwanza  tumetoka 105% mwaka 2022 hadi 109% kwa mwaka 2023, mafanikio haya yametokana na utekelezaji wa elimu bila malipo ulioanza Januari mwaka 2016,” amesema.

Kwa upande wake Afisa Elimu Awali na Msingi wa Halmshauri hiyo, Elestina Chanafi amesema kuwa wanatambua jitihada zilizofanywa na wadau mbalimbali wa sekta hiyo kitu kilicholeta mabadiliko chanya kwenye suala la ufundishaji  na kuongeza ufaulu.

“Tulitamani kuwa na siku hii maalumu kama kisababisho cha mafanikio haya ya kielimu ili tuambiane asante pamoja na kupongezana ikiwemo kuweka mikakati ya kuwa bora zaidi ya hivi tulivyokuwa leo,” amebainisha.

Katika hatua nyingine mwakilishi wa Mwenyekiti wa halmshauri hiyo, Laurent Poteza alishauri kwa mwaka unaofuata kuwajumisha wanafunzi waliofanya vizuri katika mitihani mbalimbali ya upimaji kitaifa ili kuwatia hamasa.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • PAMBA KUINUA UCHUMI WA WAKULIMA

    May 08, 2025
  • WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WAHASWA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.