• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

WAANDISHI WA HABARI MKOANI KIGOMA KUHAMASISHA ELIMU BORA KWA WOTE

Posted on: January 16th, 2023

Na Mwandishi Wetu

Wamiliki wa  vyombo vya habari na waandishi wa habari Mkoani Kigoma wametakiwa kushirikiana na Jamii katika kukuza Viwango vya elimu Mkoani hapo 


Wadau hao wa habari wametakiwa na Katibu Tawala Msaidizi idara ya elimu Mkoa wa Kigoma  Bi. Paulina Ndigezà  akimuwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa  huo January 16, 2023 katika kikao kilichofanyikia Ukumbi wa Hoteli ya Glonency uliopo Halmashauri ya Mji Kasulu  


Kikao hicho kilihusisha Wamiliki wa Vyombo vya habari, Maafisa Mawasiliano Serikalini, Maafisa elimu ngazi ya Mkoa , na Waandishi wa Habari waliopo Mkoani hapo 


Katika kikao hicho kiongozi huyo aliwataka wadau hao wa vyombo vya habari kuendelea kutoa taarifa na elimu kwa umma juu ya miradi inayotekelezwa Mkoani hapo ikiwemo mradi wa Shule Bora 


Aliendelea  kuwataka kuelimisha jamii kushiriki kwa kuzifanya Shule ziwajibike na kuongeza uelewa wa Jamii kuhusu umuhimu wa kila Mtoto( Kike au Kiume), na Watoto  wenye ulemavu kuandikisha na kuhudhuria Shule


Awali akiwasilisha taarifa ya Utekelezaji Afisa habari wa Mradi wa Shule Bora Ndugu. Raymond kayombo alisema mradi wa Shule bora umekuwa ukitekeleza mafunzo ya Walimu kazini (MEWAKA) kwa lengo la kuboresha suala la  Ufundishaji na Ujifunzaji 


Aidha amesema tayari Maafisa Mawasiliano Serikalini kwa ngazi ya Mikoa na Halmashauri inayotekeleza mradi wamefanya vikao na kuweka maazimio namna watakavyofanya kazi na Wamiliki wa vyombo vya habari pamoja na  Waandishi  wa Habari katika kuboresha utoaji wa taarifa za mafanikio 


Alisema katika utekelezaji wa mradi wa Shule bora Wajibu wa Wamiliki wa vyombo vya habari na waandishi wa habari ni kuibua changamoto na uelimishaji wa jamii katika maeneo yanayotekelezwa na mradi ikiwemo suala la Ufundishaji , Mazingira salama ya kujifunzia, Elimu jumuishi, Ufaulu na Mdondoko wa wanafunzi


Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Ofisi ya Rais TAMISEMI  Ndugu. Fred Kibano aliwataka  Waandishi wa Habari  kutumia kalamu zao kufikisha ujumbe kwa jamii kupitia Uandishi wa Habari, makala,  uandaaji wa vipindi kupitia vyombo vyote vya habari ikiwemo magazaeti, radio, televisheni,  na mitandao ya kijamii ili kufikisha ujumbe kwa makundi mbalimbali  


Naye Katibu Msaidizi wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mkoani Kigoma Ndugu. Jackson Ruvilo alisema Waandishi wa habari wataendelea kushirikiana na Serikali kupitia Mradi wa Shule Bora  kuhabarisha na kuelimisha jamii kuhakikisha Watoto wanapata elimu bora kupitia Wadau mbalimbali wakiwemo Jamii, Wazazi, Walimu na Mamlaka zinazosimamia elimu Mkoani hapo   


Miradi wa Shule bora unatekelezwa katika Mikoa tisa (9) Nchini Tanzania ukihusisha Halmashauri sitini na saba (67) na Shule elfu tano  mia saba hamsini na saba   ( 5, 757) na Unatarajia kuwanufaisha Wanafunzi zaidi ya Milioni tatu na laki nane ( 3, 800,000) na Walimu zaidi ya  elfu hamsini na nne ( 54, 000) 


Mikoa inayotekeleza mradi wa Shule bora ni pamoja na Mkoa wa Kigoma, Katavi, Dodoma, Mara, Pwani,  Rukwa, Simiyu, Singida na Mkoa wa Tanga

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • PAMBA KUINUA UCHUMI WA WAKULIMA

    May 08, 2025
  • WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WAHASWA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.