• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

UYOGA SOKO LAKE NI LA UHAKIKA- TAFITI

Posted on: December 22nd, 2023

Na Mwandishi Wetu 

Tafiti iliyofanyika katika Wilaya ya Kasulu  mkoani Kigoma imebaini kilimo cha zao la Uyoga kitawanufaisha wananchi wa eneo husika kwakuwa uhitaji wake ni mkubwa katika soko.

Hayo yamebainishwa hivi karibuni na Mkufunzi Mwandamizi  kutoka Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO), Halima Kazindolo kwenye warsha ya wadau kuhusu tathimini ya mradi wa uzalishaji  wa Uyoga katika wilaya hiyo.

Amesema kabla ya kuanza utekelezaji wa kilimo hicho ni lazima hamasa itolewe kwa wakulima kuwa kuna uhakika wa soko pamoja na kuchukua muda mfupi wa  hadi kukamilika kwake.

“Uyoga ni zao linalokaa kwa muda mfupi sisi wataalamu tunaweza kusema  ni namna gani tunaweza kuliongezea uhai ili liweze kufika katika masoko mengine ambapo huko  kilo moja bei inaanzia shilingi elfu nane hadi ishirini,” amesema.

Pia, amebainisha kuwa tafiti hiyo imebaini zao hilo linapendwa na watu wapo tayari kulilima, kitu kitakachosaidia upatikanaji wake na kuachana na ule wa kienyeji ambao kutokana na changamoto ya misitu kuwa kubwa upatikanaji wake umekuwa shida.

Naye Andrew Ching’ole kutoka  Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) amesema kuwa kupitia tathimini hiyo amejifunza Uyoga unalimika kipindi chote cha mwaka na kukamilika ndani ya miezi miwili kabla ya kufika sokoni.

“Nimejifunza Uyoga una faida katika masuala ya lishe kwa kuwa na vitamini nyingi kwa pamoja, madini mengi, kuimarisha ngozi, kutibu kisukari, moyo, shinikizo la damu na figo magonjwa ambayo yanatusumbua sana,” amesema.

Meneja wa SIDO Mkoa wa Kigoma, Gervas Ntahamba amebainisha kuwa tafiti hiyo imefanyika katika vijiji vinne katika wilaya hiyo na kutoka na taarifa ambayo haijakamilika hivyo kupitia uwasilishaji huo watapata maoni na mawazo kwa ajili ya maboresho.

Awali akifungua uwasilishaji huo mwakilishi wa Mkurugenzi wa Halmshauri ya Wilaya ya Kasulu,Audax Kamugisha  aliwataka washiriki kuisikiliza kwa makini tathimini hiyo ili kubaini kama imefikia malengo yaliyokusudiwa.

“Kilimo cha Uyoga ni kikubwa na chenye manufaa kwa jamii kwenye kuwaingizia pesa ila kama hujaelezwa huwezi kujua undani wake lakini tukiielewa tathimini wenzetu waliofanya tunaweza kuingia katika kilimo hiki vizuri,”amesema.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • KASULU DC YAANZISHA SHAMBA DARASA LA VIAZI LISHE KUKABILIANA NA UTAPIAMLO

    June 15, 2025
  • KUU KASULU YAKAGUA MIRADI YA MWENGE

    June 13, 2025
  • MATUMIZI YA ZANA ZA UFUNDISHAJI YATAJWA KUONGEZA UFANISI SHULENI

    June 11, 2025
  • WALIMU SHULE YA MSINGI KISUMA WATOA SHUKRANI KWA WADAU WALIOCHANGIA SARE NA VIFAA KWA WANAFUNZI

    June 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.