• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

UNHCR YAENDELEA KUISHIKA MKONO KASULU

Posted on: December 15th, 2022


Shirika la umoja wa mataifa la kuwasaidia wakimbizi duniani UNHCR, limetoa msaada wenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mia moja kwa wakazi wa kijiji cha Kagerankanda wilayani Kasulu kwa kujenga vyumba viwili vya madarasa, choo chenye matundu sita na kuweka mfumo wa maji, anaripoti Respice Swetu

 

Akitoa taarifa ya ujenzi wakati wa hafla ya kukabidhi miundombinu hiyo, mhandisi wa shirika la UNHCR aliyesimama kazi hiyo Simon Peche ameeleza kuwa jumla ya shilingi milioni mia moja kumi na mbili, laki tano na ishirini na nane elfu zimetumika.

 

Peche aliyekuwa ameambatana na maafisa wengine wa shirika hilo wakati wa makabidhiano hayo amesema kuwa, UNHCR kupitia mpango wa kusaidia maeneo yaliyoathiriwa na wakimbizi, wataendelea kusaidia maeneo hayo kadri itakavyowezekana.

 

Ameongeza kuwa msaada kama huo ulioambatana na uwekaji wa madawati kwenye vyumba hivyo, umefanyika pia katika halmashauri za wilaya ya Kibondo na Kakonko mkoani Kigoma.

 

Akipokea msaada huo kwa niaba ya Katibu Tawala wa mkoa wa Kigoma, Ofisaelimu taaluma wa mkoa huo Joas Jonas amelishukuru shirika hilo na kuwataka wakazi wa Kagerankanda kuyatunza majengo hayo.

 

"Pamoja na kuyatunza mnatakiwa kuweka utaratibu wa kuanza kuyatumia mara shule zitakapofunguliwa Januari mwaka kesho", aliagiza.

 

Miundombinu hiyo iliyojengwa kwenye eneo la shule ya msingi ya Nyanzaza iliyoanzishwa zaidi ya miaka kumi iliyopita, inakusudiwa kupunguza msongamano wa wanafunzi kwenye shule mama ya Kagerankanda uliotokana na kukosekana kwa madarasa kwenye eneo la shule ya msingi ya Nyanzaza.

 

Akizungumza katika hafla hiyo, Ofisaelimu wa halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Elestina Chanafi amesema, kupatikana kwa miundombinu hiyo kutaendeleza ufaulu wa shule hiyo ambayo katika matokeo ya mtihani wa kuhitimu darasa la saba uliofanyika mwaka jana, imefaulisha kwa zaidi ya asilimia 90.

 

Msaada huo ni mwendelezo wa shirika hilo kuishika mkono halmashauri ya Wilaya ya Kasulu ambapo katika siku za karibuni shirika hilo,  limeikabidhi halmashauri ya Wilaya ya Kasulu matundu sita ya vyoo vilivyojengwa kwenye shule ya msingi ya Kumtundu. 

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • KASULU DC YAANZISHA SHAMBA DARASA LA VIAZI LISHE KUKABILIANA NA UTAPIAMLO

    June 15, 2025
  • KUU KASULU YAKAGUA MIRADI YA MWENGE

    June 13, 2025
  • MATUMIZI YA ZANA ZA UFUNDISHAJI YATAJWA KUONGEZA UFANISI SHULENI

    June 11, 2025
  • WALIMU SHULE YA MSINGI KISUMA WATOA SHUKRANI KWA WADAU WALIOCHANGIA SARE NA VIFAA KWA WANAFUNZI

    June 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.