• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

TARATIBU ZA UTOAJI ENEO LA UWEKEZAJI KIGOMA SUGAR ZILIFUATWA-WAKAZI KASULU

Posted on: May 29th, 2019

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Kasulu akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Kigadye(hawapo pichani) wakati wa ziara ya Kamati ya Siasa ya Wilaya iliyofanyika kwa lengo la kufahamu hali halisi ya ushirikishwaji wa wananchi katika utoaji wa maeneo ya vijiji kwa Halmashauri kwa lengo la kumkodisha maeneo hayo Mwekezaji Kigoma Sugar.

Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Kanali Simon Anange akizungumza na Wananchi (Hawapo pichani) akiwa pamoja na Viongozi mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi, Wah. madiwani  na wataalam walioshiriki ziara ya Kamati ya Siasa iliyofanyika Leo Tarehe 29.5.2019.

Baadhi ya wakazi wa kijiji cha Nyarugusu waliojitokeza kukutana na kamati ya  Siasa ya Wilaya.

Na. Andrew Ginnethon-Kasulu.

Wakazi wa vijiji  vya Kiyungwe, Nyarugusu, na Kigadye wamethibitisha taratibu zilifuatwa wakati wa utoaji wa baadhi ya maeneokatika vijiji hivyo ili kuipa Halmashauri ambayo ipo kwenye mchakato wa kumkodishia Mwekezaji M/S Kigoma Sugar Company Ltd kwa ajili ya uwekezaji wa Kiwanda cha Sukari.

Hayo yamebainika leo tarehe 29.5.2019 wakati kamati ya Siasa Wilaya ya Kasulu ilipofanya ziara na kuongea na wananchi kwenye vijiji hivyo, kwa kushirikiana na Wajumbe wa Kamati ya Fedha pamoja na wataalam wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu.

Kamati hiyo imewahoji baadhi ya wananchi waliokua wajumbe wa mabaraza ya Ardhi pamoja na viongozi mbalimbali waliowahi kushika nyadhifa kwenye vijiji  hivyo, ambapo wamethibitisha kuwa taratibu zote ikiwemo Mikutano ya vijiji na ushirikishwaji wa kila hatua vilifanyika.

Mkuu wa Wilaya ya Kasulu, Kan. Simon Anange, amewasisitiza wakazi wa vijiji hivyo kuwa wawazi mbele ya Kamati, kuhusu suala zima la utoaji wa Maeneo hayo kwa Halmashauri kwa Lengo la uwekezaji. “Tumekuja ili kamati ya Siasa ya wilaya, ijiridhishe kuhusu taratibu zilizotumika katika upatikanaji wa maeneo ya uwekezaji ya Kigoma Sugar”

Amewataka wananchi hao  kuyapuuza maneno ya upotoshaji yanayoenezwa na baadhi ya wananchi kuwa maeneo hayo yana mgogoro huku wakiwa na lengo la kuchelewesha au kuzuia uwekezaji kwa manufaa yao binafsi ikiwemo ufugaji usiofuata utaratibu.

Kan. Anange amesema uwepo wa Kiwanda hicho cha Sukari utasaidia kupatikana kwa ajira za kudumu zaidi ya 600 na amewataka wakazi hao waachane na utaratibu wa kuuza ardhi bila sababu za msingi.

Akitoa ufafanuzi kwa Wajumbe wa kamati ya siasa wilaya, Mkurugenzi Mtendaji Mha. Godfrey Kasekenya, amesema wananchi watapata fursa ya kulima miwa na kupatiwa Pembejeo na Mwekezaji kisha watarejesha gharama wakati wa mauzo. 

Amesema kuwa, eneo hilo halina mgogoro kwa sababu wakazi wachache waliokuwa wakiishi kinyume na utaratibu, walishatengewa eneo  lenye zaidi ya Hekta 1000 katika kitongoji cha Mkuyuni kilichopo kata ya Nyamidaho.

Mwenyekiti wa CCM wilaya, Ngd Mbelwa Abdallah, amepongeza utaratibu wa ushirikishwaji uliofanyanyika ambapo umepelekea Kamati ya siasa kuwa na uelewa wa pamoja kuhusu masuala ya kiutekelezaji Ilani ya Chama cha Mapinduzi.

“Utaratibu huu unapelekea kuondoa shaka na kupata nafasi ya Chama cha Mapinduzi ambacho ndicho chenye dhamana ya kuongoza Nchi,  kuona na kushauri juu ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo. Tumejiridhisha kuwa taratibu za upatikanaji maeneo zimefuatwa na sisi kama Chama tumebariki taratibu zinazofuata ziendelee” amehitimisha Mbelwa.

Ndg. Riziki Gervas ambaye ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyarugusu, amesema mikutano mbalimbali ya kisheria ilifanyika na wananchi walishirikishwa kila hatua, Muhtasari uliandikwa na wananchi  wanao uelewa wa kutosha kuhusu suala la mwekezaji.

Ziara hiyo imehitimishwa kwa kamati kutembelea Kituo cha Afya Nyamidaho pamoja na kukagua maendeleo ya ujenzi wa Majengo ya Hospitali ya Wilaya ya Kasulu. Katika kituo cha afya Nyamidaho, kamati imekagua na kushuhudia utekelezaji ma maagizo ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge  2019 Ndg. Mzee Mkongea Ali, aliyeagiza kufanyika marekebisho kadhaa kwenye majengo ya Kituo cha Afya Nyamidaho. Kamati imekagua na kuridhika na marekebisho yaliyofanyika kisha kutoa pongezi kwa uongozi wa Halmashauri kwa utekelezaji.

Ikiwa kwenye Mradi wa ujenzi wa Hospitali ya wilaya, kamati  imekagua na  kuona maendeleo ya ujenzi wa majengo mbalimbali na kutoa ushauri juu ya masula kadhaa ya kiutendaji.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • KASULU DC YAANZISHA SHAMBA DARASA LA VIAZI LISHE KUKABILIANA NA UTAPIAMLO

    June 15, 2025
  • KUU KASULU YAKAGUA MIRADI YA MWENGE

    June 13, 2025
  • MATUMIZI YA ZANA ZA UFUNDISHAJI YATAJWA KUONGEZA UFANISI SHULENI

    June 11, 2025
  • WALIMU SHULE YA MSINGI KISUMA WATOA SHUKRANI KWA WADAU WALIOCHANGIA SARE NA VIFAA KWA WANAFUNZI

    June 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.