• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

MKUU WA MKOA KIGOMA AWEKA JIWE LA MSINGI KITUO CHA AFYA NYAMIDAHO.

Posted on: August 11th, 2018

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kasulu(wa pili kulia) Mhandisi Godfrey Kasekenya akifurahia jambo wakati wa sherehe ya uwekaji jiwe la msingi katika kituo cha afya cha Nyamidaho. Kushoto kwake ni Mh. Said Ndiyunze Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya Kasulu.

Mkurugenzi wa Hamlmashauri ya wilaya ya  Kasulu Mhandisi Godfrey Kasekenya akipokea zawadi kutoka kwa watumishi wa Kituo cha Afya Nyamidaho katika kuonnyesha na kuthamini bidii pamoja na mchango wake katika kusimamia na kuhakikisha ujenzi wa Kituo cha Afya Nyamidaho unafanyika na kukamilika.


Na,Andrew Mlama.Kasulu.

Mkuu wa Mkoa wa Kigoma  Brigedia Jenerali mstaafu Emmanuel Maganga, ameweka jiwe la msingi katika kituo cha Afya Nyamidaho ambacho hapo awali ilikua ni Zahanati kisha kupanuliwa na  kupandishwa hadhi kuwa kituo cha Afya ambapo ujenzi wake umegharimu Sh. 5,37,800,000 ambapo sh. Mil 500 ni kutoka serikali kuu na kiasi kilichobaki ni nguvu za wananchi pamoja na mchango kutoka halmashauri.

Uwekaji huo wa jiwe la msingi umefanyika leo tarehe 11.08.2018 katika kata ya Nyamidaho iliyopo wilayani hapa, ambapo zimefanyika kazi za ujenzi wa miundombinu na majengo sita ikiwemo jengo la maabara, wodi ya wajawazito na watoto, jengo la upasuaji, jengo la kuhifadhia maiti, jengo la wagonjwa wa nje na nyumba ya mganga.

Baada ya uwekaji jiwe la msingi ,amekagua majengo hayo ambayo ukamilifu wake umetimia kwa 98%, amesisitiza uwepo wa akina baba wakati wake zao wanapojifungua ili nao waweze kuhisi, kusikia na kuona uzito wa tendo la uzazi unaowakabaili wake zao. Amesisitiza watumishi na wananchi kuyatunza majengo hayo ili yaweze kudumu na ameridhishwa kwa kiasi kikubwa na ujenzi huo.

Katika hotuba yake baada ya uwekaji jiwe la msingi, mkuu wa mkoa wa Kigoma amewashukuru wananchi kwa kujitolea akiba ya  Matofali 48,000, kuchimba mtaro na kuweka mabomba ili kuhakikisha kituo kinapata maji ya uhakika. “katika maendeleo hakuna Siasa , wananchi fanyeni maendeleo kwani utoaji na upatikanaji wa huduma haujali vyama” amesisitiza Maganga.

Amewataka wanajamii kuishi kwa kiasi ikiwemo kula, kunywa na kujenga tabia ya kuridhika pamoja na kufanya mazoezi ya mara kwa mara kwa lengo la kuimarisha  Afya na kudumisha utimamu wa miili na kupelekea utendaji na utekelezaji mzuri wa majukumu ya kila siku kwa maendeleo yao.

Amewataka wananchi kuendelea kuunga mkono Chama Cha Mapinduzi ili kuhakikisha sera zake zinatekelezwa. Aidha amewahakikishia kutekeleza maombi yote waliyo yatoa kwake awamu kwa awamu na ikiwemo uwekaji wa umeme katika kituo hicho cha Afya jambo ambalo amelikabidhi kwa mbunge wa Kasulu vijijini Mh. Augustino Vuma.

Akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi, Mkurugenzi mtendaji wa Halmahsauri  ya wilaya Kasulu Mhandisi Godfrey Kasekenya, amesema kuwa halmashauri imetenga zaidi y ash. Mil 5 kwa ajili ya ujenzi wa magati mawili eneo ambalo bomba la maji  la kituo cha Afya limepita kwalengo la kutoa huduma ya maji safi  kwa wananchi.

Aidha amemuomba mkuu wa mkoa asaidie kufikisha serikalini maombi ya kusaidiwa kufanikisha ujenzi wa nyumba za watumishi, ujenzi wa wodi ya wanawake, watoto na wanaume, jengo la kufulia nguo pamoja na kuweka msukumo ili kuweka umeme katika majengo na kupatikana kwa jenereta itakayotumika itakapotokea dharura  ya kukatika kwa umeme.

Akisoma taarifa ya ujenzi wa mradi huo, Kaimu mganga mkuu wa wilaya ya Kasulu Bw. Mageni Pondamali amesema kuwa huduma zitakazotolewa katika kituo hicho ni pamoja na huduma ya upasuaji kwa akina mama wanaoshindwa kujifungua,upatikanaji vipimo vya msingi, kuhifadhi maiti na makazi bora kwa watumishi wa Afya. Amesema ujenzi umekamilika kwa 98%. Amesema mradi huo utakapokamilika utahudumia watu  1,76,212 wa tarafa ya Makere.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • KASULU DC YAANZISHA SHAMBA DARASA LA VIAZI LISHE KUKABILIANA NA UTAPIAMLO

    June 15, 2025
  • KUU KASULU YAKAGUA MIRADI YA MWENGE

    June 13, 2025
  • MATUMIZI YA ZANA ZA UFUNDISHAJI YATAJWA KUONGEZA UFANISI SHULENI

    June 11, 2025
  • WALIMU SHULE YA MSINGI KISUMA WATOA SHUKRANI KWA WADAU WALIOCHANGIA SARE NA VIFAA KWA WANAFUNZI

    June 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.