• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

MAGHALA KUSAIDIA USIMAMIZI WA MAZAO NA SOKO KWA WAKULIMA

Posted on: December 16th, 2023

Na Mwandishi Wetu

Serikali imesema kuwa ujenzi wa  maghala ya kisasa yapatayo 14 kote nchini yataliwezesha taifa kutoka hatua moja kwenda nyingine  kwenye suala la usimamizi wa mazao ya chakula huku wakulima wakiwa na   uhakika wa soko.

Hayo yamebainishwa juzi na Mratibu wa kudhibiti Sumu Kuvu nchini, Clepin Josephat katika Kijiji cha Nyakitonto wilayani Kasulu mkoani Kigoma kwenye makabidhiano ya miundombinu ya mradi wa uthibiti wa sumu hiyo.

Amesema ghala hilo la Nyakitonto lililogharimu kiasi cha shilingi bilioni 1.1 lina uwezo kukusanya mazao ya nafaka tani 2000 kitu kitakachowasaidia wakulima kuepeukana na wadudu waharabifu baada ya mavuno.

Mkurugenzi Wa Mafunzo na Utafiti Wizara ya Kilimo, Dk Wilhelm Mafuru  aliyemwakilisha Katibu Mkuu, Gerald Mweli amesema kuwa wizara imeupatia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula  (NRFA) usimamizi wa ghala hilo kutokana na uzoefu waliokuwa nao katika masuala ya ukusanyaji wa chakula.

“ Serikali inatarajia mtatoa elimu kwa wakulima kupitia wataalamu wenu kwakuwa huwa mnanunua bidhaa ambazo ni bora, kwahiyo mtatumia wataalamu wenu kuwasaidia wakulima kuzingatia kanuni bora za kilimo,” alisema.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmshauri ya Wilaya ya hiyo, Emmanuel Ladislaus   aliiomba wizara kuangalia maeneo mengine yanayoweza kujengwa maghala kutokana na jiografia ya eneo hilo kuwa na uzalishaji mkubwa wa mazao ya nafaka.

“ Wilaya yetu ni moja ya wilaya zinazozalisha nafaka kwa kiasi kikubwa jaribuni kuangalia suala la kutujengea maghala kwakuwa tuna uzalishaji mkubwa kwahiyo niwaombe serikali mtuongezee idadi yake,” amesema.

Diwani wa Kata ya Nyakitonto, Daniel Mzababa amesema kuwa uwepo wa ghala hilo utasaidia kuongeza mnyororo wa thamani wa mazao yao kwakuwa  kijiji hicho kinaongoza kuhudumia wafanyabiashara kutoka  nchi za Kenya, Burundi, Rwanda na Uganda wanaofuta bidhaa za nafaka.


Serikali kwa kushirikiana na Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB) na Mfuko wa Dunia wa Kusaidia Usalama wa Chakula (GAFSP) tayari imejenga maghala 12 Tanzania Bara na mawili Zanzibar yenye thamani ya shilingi bilioni 14.3 kwa ajili ya uhifadhi wa chakula.




Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • KASULU DC YAANZISHA SHAMBA DARASA LA VIAZI LISHE KUKABILIANA NA UTAPIAMLO

    June 15, 2025
  • KUU KASULU YAKAGUA MIRADI YA MWENGE

    June 13, 2025
  • MATUMIZI YA ZANA ZA UFUNDISHAJI YATAJWA KUONGEZA UFANISI SHULENI

    June 11, 2025
  • WALIMU SHULE YA MSINGI KISUMA WATOA SHUKRANI KWA WADAU WALIOCHANGIA SARE NA VIFAA KWA WANAFUNZI

    June 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.