• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

ALAT MKOA WA KIGOMA WAMPA TANO MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

Posted on: May 14th, 2022





Wajumbe wa jumuiya za serikali za mitaa ALAT mkoa wa Kigoma, wametoa pongezi kwa mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kasulu Joseph Kashushura kutokana na kazi nzuri anayoifanya kusimamia matumizi ya pesa za serikali na zinazotokana na mapato ya ndani katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo kwenye halmashauri hiyo.

Pongezi hizo wamezitoa mwishoni mwa wiki walipokuwa katika ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya ujenzi inayotekelezwa katika halmashauri ya wilaya ya Kasulu.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, mwenyekiti wa ALAT mkoa wa Kigoma Jackson Mateso amesema, kinachofanywa na mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, kinapaswa kuigwa na wakurugenzi wa halmashauri zote za mkoa wa Kigoma.

Kutolewa kwa kauli hiyo, kumetokana na taarifa iliyosomwa kwenye ziara hiyo ikionesha kuwa, halmashauri ya wilaya ya Kasulu imetumia zaidi ya shilingi milioni mia mbili kutokana na pesa za mapato ya ndani kujenga nyumba tano za watumishi wa idara ya afya.

"Sasa hapa kila mkurugenzi anaona, wakurugenzi wote wa halmashauri za mkoa wa Kigoma mnaona, tunaposema kuwa pesa zinazotokana na makusanyo ya ndani zinaweza kufanya kitu kikafanikiwa mfano wake tunauona hapa, hongera sana Mkurugenzi kwa maono yako na maono hayo yaendelee", amesema Mateso.

Pamoja na kutembelea ujenzi wa nyumba tano za watumishi, miradi mingine iliyofikiwa na ugeni huo ni ujenzi wa jengo la makao makuu ya halmashauri na wodi tatu za wagonjwa zinazoendelea kujengwa katika hospitali ya halmashauri ya wilaya ya Kasulu.

Ziara hiyo ilifuatiwa na kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa halmashauri ya Wilaya ya Kasulu.

Akizungumza wakati wa kuahirisha kikao hicho, Mateso amewataka wajumbe wa kikao hicho kuzitumia ziara wanazozifanya kuwa na manufaa kwa kubadilishana mawazo, uzoefu na kudumisha mshikamano.

Mateso ambaye pia ni mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Uvinza, amewataka wajumbe wa ALAT mkoa wa Kigoma kushiriki kikamilifu katika kufanikisha sensa ya watu na makazi itakayofanyika Agosti 23, mwaka huu.



Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • KASULU DC YAANZISHA SHAMBA DARASA LA VIAZI LISHE KUKABILIANA NA UTAPIAMLO

    June 15, 2025
  • KUU KASULU YAKAGUA MIRADI YA MWENGE

    June 13, 2025
  • MATUMIZI YA ZANA ZA UFUNDISHAJI YATAJWA KUONGEZA UFANISI SHULENI

    June 11, 2025
  • WALIMU SHULE YA MSINGI KISUMA WATOA SHUKRANI KWA WADAU WALIOCHANGIA SARE NA VIFAA KWA WANAFUNZI

    June 05, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.