• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

VIONGOZI WA CCM MKOA WAFANYA ZIARA KASULU

Posted on: March 12th, 2022

Mkuu wa Wilaya ya Kasulu Kanali Isack Mwakisu (aliyesimama) akizungumza katika kikao  cha viongozi wa chama cha Mapinduzi mkoa wa Kigoma kilichofanyika Wilayani Kasulu, walioketi ni Katibu Mwenezi wa CCM mkoa wa Kigoma Feruzi Mbaya (kushoto);na Katibu wa CCM Mkoa wa Kigoma Mobutu Malima.


MKUU wa Wilaya ya Kasulu Kanali Isack Mwakisu, amewatahadharisha wakazi wa Wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma kuepuka vitendo vyovyote vinavyoweza kukwamisha zoezi la anuani za makazi.

Kauli hiyo ameitoa katika kikao kilichowahusisha viongozi wa Chama cha Mapinduzi wa mkoa wa Kigoma walipokuwa wakihitimisha ziara ya siku mbili Wilayani Kasulu.

Mwakisu ametoa  kauli hiyo kufuatia baadhi ya hoja zilizowasilishwa katika kikao hicho kuhusu migogoro ya mipaka iliyopo katika vijiji na mitaa ya wilaya ya Kasulu.

Amesema kuwa, mipaka hiyo kamwe isihusishwe na anuani za makazi na  atakaposikia kuna mtu yeyote katika Wilaya hiyo  amesababisha kukwama kwa zoezi la anuani za makazi, atamchukulia hatua kali  ikiwa ni pamoja na kumweka ndani.

“Rais wetu amekwisha toa pesa nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa zoezi la anuani za makazi, siko tayari kusikia kuwa kuna mtu anakwamisha zoezi hilo”, alisema.

Akizungumzia suala la wakimbizi wanaoingia nchini bila utaratibu, Kanali Mwakisu amewataka wakazi wa Wilaya ya Kasulu  kushirikiana na serikali katika kukabiliana na tatizo hilo badala ya kuitegemea idara ya uhamiaji na vyombo vya usalama pekee kwa kuwa jukumu la ulinzi na usalama wa nchi ni la kila raia.

Ameongeza pia kuwa, tatizo la wahamiaji kutoka nchi jirani ni moja ya matatizo makubwa yaliyopo katika Wilaya ya Kasulu hivyo vyombo vya ulinzi pekee havitaweza kutokana na ukubwa wa tatizo hilo.

Awali katika kikao hicho, Katibu wa Chama cha Mapinduzi wa mkoa wa Kigoma Mobutu Malima, amewaasa  wataalamu na viongozi wa siasa Wilayani Kasulu kushirikiana kwa pamoja katika kutekeleza ilani ya Chama cha Mapinduzi.

Amesema kuwa, kazi ya viongozi wa  Chama ni kuhakikisha kuwa ilani ya Chama inatekelezwa na kazi ya wataalamu ni kutekeleza ilani ya Chama.

Aidha, Malima ambaye ziara hiyo ni ziara yake ya kwanza Wilayani Kasulu tangu ateuliwe kushika wadhifa huo mwishoni mwa mwaka jana,  ametoa pongezi kwa  viongozi wa Wilaya hiyo kwa kazi  wanazofanya.

Kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri ya mji wa Kasulu,  kimewakutanisha wataalamu, wanasiasa na madiwani wa Halmashauri na mji wa Kasulu.

Picha ya pamoja ya viongozi wa Chama cha mapinduzi na wataalamu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu.



Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • PAMBA KUINUA UCHUMI WA WAKULIMA

    May 08, 2025
  • WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WAHASWA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.