• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

TANZANIA NA BURUNDI ZAANZA RASMI UJENZI WA RELI YA KISASA YA UVINZA-MUSONGATI

Posted on: August 16th, 2025

Na Mwandishi Wetu 

Serikali za Tanzania na Burundi leo, Jumamosi Agosti 16, 2025, zimeweka jiwe la msingi kuashiria kuanza kwa ujenzi wa Reli ya Kisasa ya Mwendokasi (SGR) kutoka Uvinza mkoani Kigoma hadi Musongati nchini Burundi, yenye urefu wa kilomita 300.

 Mradi huo unakadiriwa kugharimu dola bilioni 2.154 na unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 72, sawa na miaka sita.

Akizungumza kwenye hafla iliyofanyika Musongati, Rais wa Burundi, Mhe. Évariste Ndayishimiye, ameishukuru Tanzania kwa mchango wake mkubwa katika maendeleo na usalama wa nchi hiyo.

Amesema ujenzi wa reli hiyo utakuwa kichocheo cha kiuchumi kwani utarahisisha usafirishaji wa malighafi kutoka Bandari ya Dar es Salaam kuelekea migodi ya Nikeli iliyoko Musongati, na kisha kusafirishwa kwenda masoko mbalimbali duniani.

“Nashukuru Tanzania kwa kuwa mdau mkubwa wa maendeleo nchini kwetu. Tayari imetupatia bure sehemu ya Bandari Kavu Kigoma kwa ajili ya mizigo, na pia kiwanja eneo la Kwara, mkoani Pwani, kitakachotumika kujenga Bandari Kavu,” amesema Rais Ndayishimiye.

Kwa upande wake, Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, aliyemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amesema mradi huo ni sehemu ya utekelezaji wa ajenda ya Umoja wa Afrika inayolenga kuhakikisha ifikapo mwaka 2063 bara lote linakuwa na mtandao bora wa miundombinu ya usafirishaji.

“Reli hii itafungua fursa nyingi za kiuchumi kwa wananchi wetu. Kwa mfano, safari ya kutoka Bujumbura hadi Dar es Salaam kwa sasa huchukua saa 96 kwa gari, lakini kupitia reli hii itapungua hadi saa 20 pekee. Hii itapunguza gharama za usafirishaji kwa zaidi ya 40%,” amesema Majaliwa.

Awali, Waziri wa Uchukuzi wa Tanzania, Mhe. Prof  Makame Mbarawa, amebainisha kuwa reli hiyo itakapo kamilika itakuwa na uwezo wa kusafirisha tani 3,800 za mizigo kwa wakati mmoja, hatua itakayopunguza gharama na ushuru wa bidhaa kati ya nchi hizo mbili jirani.


Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MPANGO WA UWAWA WAIBUA MATUMAINI MAPYA KATIKA SEKTA YA ELIMU KASULU

    August 20, 2025
  • MSAADA WA JKT WAOKOA ZAIDI YA MILIONI 13 KWA SHULE YA MGOMBE

    August 18, 2025
  • TANZANIA NA BURUNDI ZAANZA RASMI UJENZI WA RELI YA KISASA YA UVINZA-MUSONGATI

    August 16, 2025
  • WATUMISHI HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU WAMPONGEZA MKURUGENZI KAFUKU KWA KUSIKILIZA KERO ZAO HADI NGAZI YA KATA

    August 14, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.