• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

NYUMBA TANO ZA WATUMISHI IDARA YA AFYA ZAKAMILIKA KASULU DC

Posted on: January 10th, 2023


Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu imekamilisha ujenzi wa nyumba tano za watumishi wa Afya zilizojengwa katika hospitali ya halmashauri hiyo kwa lengo la kuboresha utoaji wa huduma na kutoa motisha kwa watumishi  hao kwa kuwapa makazi bora na salama

Nyumba hizo zilizogharimu kiasi cha shilingi Mil.290 zimejengwa kwa fedha zitokanazo na mapato ya ndani ya Halmashauri kwa awamu ya kwanza ili kutatua changamoto ya upatikanaji wa nyumba bora za watumishi  na kupunguza malalamiko katika utoaji wa huduma kwani watumishi walikua wakilazimika kutembea umbali wa kilomita 18 ili kufika katika Kituo cha kazi.

Akizungumzia ukamilishaji  wa nyumba hizo Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Dkt. Robert Nelson Rwebangira  alisema kuanzia mwaka 2023 wananchi wategemee kupata huduma bora zaidi  kwani watoa huduma watakuwa wakipatikana kwa urahisi kutokana na utatuzi wa changamoto ya ukosefu wa nyumba bora za watumishi.

"Kilichotusukuma kujenga nyumba hizi ni kwa Kata za karibu Nyakitonto na Nyamnyusi ni ngumu sana kupata nyumba bora, lengo kuu la kujenga nyumba hizi ni kuhakikisha huduma za afya za dharula zinapatikana masaa yote 24 kwa muda muafaka  watoa huduma watapatikana kiurahisi kushughulikia dharula kwa wakati lakini pia ni motisha kwa watumishi kuwapa makazi bora ambayo ni salama", alisema Rwebangira

Aliongeza kuwa kukosekana kwa makazi kwa watumishi wa kada hiyo kulikuwa kunaleta changamoto ya gharama kubwa ya utoaji wa huduma za dharula kwa wagonjwa pia malalamiko mengi kutoka kwa wananchi  kwa kukosa huduma kwa wakati muafaka hivyo nyumba hizo zitasaidia kupunguza vilema na vifo kwa wanaopata ajali vilevile kuzuia vifo kwa wamama na watoto

Kwa upande wake Mhandisi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Eng. Athanasi Nziganyije Msuta alimshukuru Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Ndugu Joseph Kashushura Rwiza kwa kujali na kuwapatia watumishi wa Idara ya Afya makazi bora na salama

Alitoa rai kwa wananchi wote wa halmshauri ya Wilaya ya Kasulu kuunga mkono shughuli zote za maendeleo zinazofanywa katika halmashauri hasa katika swala zima la ukusanyaji wa mapato ili kuleta maslahi mapana ya halmashauri na nchi kwa ujumla.

Halmashauri Ya Wilaya Ya Kasulu inatarajia kuendeleza ujenzi wa nyumba 4 za watumishi wa Idara ya Afya katika awamu ya pili zenye uwezo wa kubeba familia tatu katika kila nyumba na kutenga kiasi cha fedha shilingi 133,843,463.17 kwaajili ya ujenzi huo,  nyumba za Wakuu wa Idara zote, kituo cha Polisi na nyumba za Polisi katika Kata ya Nyakitonto kupitia mapato ya ndani.


 

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • PAMBA KUINUA UCHUMI WA WAKULIMA

    May 08, 2025
  • WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WAHASWA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.