• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

MKUTANO WA BARAZA LA MADIWANI ROBO YA TATU 2017/2018 WAFANYIKA KASULU.

Posted on: May 24th, 2018


Waheshimiwa Madiwani  pamoja na wageni mbalimbali waliohudhuria, wakifuatilia jambo wakati Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Kasulu ukiendelea.

Na. Andrew Mlama

Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu  robo ya tatu kwa mwaka 2017/2018, umefanyika leo ambapo viongozi mbalimbali toka vyama vya siasa, madhehebu ya dini, vyombo vya ulinzi na usalama, wananchi toka kata mbalimbali pamoja na wakuu wa Idara na Vitengo wamehudhuria.

“Akifungua Mkutano huo, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya Mh. Yohana Mshita, amewataka Madiwani kushirkiana na wananchi kwa ukaribu katika kusimamia maendeleo ili kuhakikisha Halmashauri inasonga mbele. “Hakikisheni mnawashirikisha wananchi na mawazo yao yafanyiwe kazi, hii itaamsha ari ya kujitolea katika utekelezaji wa shughuli za Maendeleo’’ alisisitiza Mshita.

Akijibu swali la Papo kwa papo lililoulizwa na Diwani wa Kata ya Bugaga Mh. Fidel Mtemwa ambapo alitaka kufahamu, Halmashauri inampango gani katika kuhakikisha bei za mazao zinapanda na kumnufaisha mkulima. Akijibu swali hilo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Mhandisi Godfrey Kasekenya, amesema suala hilo ni la kisera kwani linahusu  nchi nzima.

“Serikali hairuhusu mazao ya chakula kuuzwa nje ya nchi mpaka ijiridhishe na kuhakikisha  kinatosheleza Mikoa yote nchini. Upo mpango wa kujenga ghala kubwa la mazao wilayani hapa kwani wakulima huuza mazao wanayoyapata wakati wa mavuno kutokana na kukosa miundombinu mizuri ya kuhifadhia ili  kuyauza baadae kwa bei yenye faida” alihitimisha Kasekenya.

Akichangia uwasilishwaji wa Taarifa ya Kamati ya Kupambana na kudhibiti UKIMWI, Kaimu Afisa Maendeleo  ya Jamii Wilaya Bi.Victoria Makyao amesema ili Jamii iendelee lazima iwe na Afya njema. Suala la UKIMWI lizungumzwe katika Jamaii bila kificho. Wazazi wazungumze na watoto wao ili waweze kuchukua tahadhari dhidi ya UKIMWI.

Amewataka wananchi wawe makini kipindi hiki cha mavuno kwani kunamuingiliano mkubwa wa wageni toka mikoa mbalimbali wanaokuja kufanya biashara ya mazao. aidha amewakumbusha wakulima  wa kasulu  kutimimiza malengo yao mara baada ya kuuza mazao badala ya kujihusisha na masuala ya starehe.

Baraza la madiwani limepitisha pendekezo la eneo la Makao Makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, ambapo Wajumbe kwa pamoja walikubaliana eneo lililopo  katika Kata za Nyamnyusi na Nyakitonto litumike. “Eneo hilo ni katikati kuendana na Jiografia ya Wilaya yetu pia linafikika  kutoka kata zote zilizopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu” alisisitiza Mh. Hosea Nyamwombo Diwani wa Kata ya Buhoro.

Wanachi waliohudhuria wamepongeza uendeshwaji wa Mkutano wa Baraza la Madiwani, wamesema kuwa Madiwani ambao ndio wawaakilishi wao wamechangia michango yao kwa weledi, kisha kujibiwa hoja zao kwa umakini. Hali hiyo imewapa Imani juu ya  uendeshwaji wa shughuli za Kiserikali katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu.

Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • WALIMU SHULE YA MSINGI KISUMA WATOA SHUKRANI KWA WADAU WALIOCHANGIA SARE NA VIFAA KWA WANAFUNZI

    June 05, 2025
  • MAFUNZO YA SIKU TATU YA KKK KWA WALIMU WA DARASA LA KWANZA NA LA PILI YAFIKIA TAMATI KASULU

    June 05, 2025
  • KASULU DC YAENDELEA KUWAJENGEA UWEZO WALIMU WA MADARASA YA AWALI

    June 03, 2025
  • VIONGOZI WA TAASISI ZA ELIMU NA IDARA YA AFYA KASULU WATAKIWA KUSIMAMIA USAFI WA MAZINGIRA

    June 02, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.