Na Mwandishi Wetu
Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kasulu, mkoani Kigoma, imefanya ziara ya ukaguzi wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, ambayo inatarajiwa kupitiwa na Mwenge wa Uhuru mwaka 2025 kwa ajili ya uwekaji wa jiwe la msingi au uzinduzi.
Ukaguzi huo umefanyika jana, Juni 12, 2025, ambapo miongoni mwa miradi iliyokaguliwa ni pamoja na Mradi wa Kipandishio cha Makere, ujenzi wa nyumba mbili za walimu (nyumba za mbili kwa moja) katika Shule ya Sekondari Kasasa, Mradi wa Maji katika Kata ya Nyakitonto, na Mradi wa Vijana wa AGRIDOT unaohusika na usambazaji wa pembejeo za kilimo kwa wakulima wadogo.
Miradi mingine ni pamoja na ujenzi wa nyumba mbili za wakuu wa idara na vitengo katika makao makuu ya halmashauri, jengo la Mama, Baba na Mtoto (RCH) katika Hospitali ya Wilaya ya Halmashauri hiyo,ujenzi wa shule mpya ya sekondari Luhunga pamoja na mradi wa ujenzi wa barabara ya changarawe kutoka Kasangezi hadi Kigembe yenye urefu wa kilomita 10.38.
HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
Anuani ya Posta: S.L.P 97
Simu ya Mezani: +255-028-2810339
Simu: +255-028-2810339
Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz
Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.