• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe ya Ofisi |
Kasulu District Council
Kasulu District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • Misingi Mikuu
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Utawala na Utumishi
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Maji
      • Kilimo-Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo na Ustawi wa Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Manunuzi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
    • Muundo wa Utawala
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Elimu
    • Afya
    • Maji
    • Kilimo
  • Madiwani
    • Orodha ya Madiwani
    • Kamati za Kudumu
      • Fedha, Utawala na Mipango
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
      • Mipango Miji na Mazingira
      • Uchumi, Afya na Elimu
    • Ratiba
      • Vikao vya Waheshimiwa Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi inayoendelea
      • MRADI WA UMWAGILIAJI TITYE
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogondogo
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu za Maombi
    • Taratibu
    • Huduma Kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Maktaba ya Video
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Makala
    • Matangazo

KASULU KUNUFAIKA NA MPANGO WA WFP

Posted on: December 1st, 2022

Shule za msingi katika halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, zitanufaika na mpango wa lishe shuleni unaofadhiliwa na shirika la chakula duniani WFP, anaripoti Respice Swetu.


Hayo yamebainika kufuatia shirika hilo kuanza utekelezaji wa mpango huo kwa kugawa mbegu za mahindi, maharage, mchicha na miche ya parachichi kwa shule 15 za msingi zitakazoanza kunufaika na mpango huo.


Akizungumza baada ya kukamilika kwa usambazaji wa mbegu na miche hiyo, Ofisa elimu watu wazima halmashauri ya Wilaya ya Kasulu Simon Kichumu, amezitaja shule zilizopelekewa mbegu hizo kuwa ni Nyakatoke, Nyachenda, Nyakelela, Kasasa, Muungano, Nyarugusu, Nyamuganza na Kumkambati. 


Sambamba na hizo, shule nyingine zilizomo katika awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mpango huo kuwa ni Heru Ushingo, Kigadye, Nyamiyaga, Asante Nyerere, Nkundusi, Rusesa na Kakirungu.


"Kwa kuwa kila shule itatakiwa kutoa chakula cha mchana kwa wanafunzi wake kutokana na nafaka zitakazozalishwa kupitia mpango huo, kilo 40 za mbegu ya maharage, kilo 8 za mbegu ya mahindi, miche 10 ya parachichi na mbegu za mboga mboga zimetolewa kwa shule hizo", amesema.


Ameongeza kuwa, mpango huo unaotekelezwa na WFP kwa kushirikiana na kituo cha utafiti wa mbegu TARI cha jijini Arusha, unatarajiwa kuzaa matunda kutokana utayari uliooneshwa na shule hizo wakati wa kupokea mbegu hizo.


Mpango huo unaotekelezwa katika halmashauri tatu za mkoa wa Kigoma, umeanza kwa kuzifikia shule zilizo na maeneo ya kulima yenye ukubwa wa heka mbili na nusu na kuendelea.


Pamoja na halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, halmashauri nyingine zitakazonufaka na mpango huo katika mkoa wa Kigoma ni Kasulu Mji na halmashauri ya Wilaya ya Kibondo.


Kufanikiwa kwa mpango huo, kutasadifu msemo wa wahenga wa kumpa mtu nyavu badala ya samaki waliovuliwa.


Pichani, walimu na wajumbe wa kamati ya shule ya msingi Nyakelela walipokuwa wakipokea mbegu za maharage, mahindi na miche ya miti ya parachichi kwa ajili ya utekelezaji wa mpango huo.



Matangazo

  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO ILIYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU January 08, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAHILI February 17, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI YA MWENYEKITI WA BODI YA AJIRA February 21, 2024
  • MWALIKO WA ZABUNI KUPANGISHA ENEO KWAAJILI YA MGAHAWA March 08, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • PAMBA KUINUA UCHUMI WA WAKULIMA

    May 08, 2025
  • WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA WAHASWA KUFANYA KAZI KWA BIDII

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • MAWAKALA WA VYAMA KURUHUSIWA KITUONI KATIKA ZOEZI LA UBORESHAJI WA DAFTARI LA WAPIGA KURA

    April 29, 2025
  • Angalia Zote

Video

NAIBU WAZIRI OR-UTUMISHI NOV 2022
Video zaidi

KURASA ZA KARIBU

  • PlanRep_Web_Based
  • FFARS Online Manual
  • PlanRep Online Manual
  • Facility Financial Accounting and Reporting System (FFARS)
  • safari_Live
  • safaridemo
  • Dashibodi ya Ukusanyaji wa Mapato
  • UNICEF Dashboard
  • Kamusi Eng & Swa

TOVUTI ZINAZOHUSIANA

  • TOVUTI KUU YA SERIKALI
  • TAMISEMI
  • BUNGE
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • ARIDHI
  • OPEN UNIVERSITY
  • PSPTB
  • AJIRA
  • HFR Dashboard
  • KIGOMA DC
  • NACTE
  • NECTA
  • eMrejesho

Kihesabu watembeleaji

world map hits counter

Wasiliana Nasi

    HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU

    Anuani ya Posta: S.L.P 97

    Simu ya Mezani: +255-028-2810339

    Simu: +255-028-2810339

    Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Visitors Counter

writingMasterThesis

    • Sera Ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani
    • Huduma
    • Wasiliana Nasi

Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.