Na Mwandishi Wetu
Halmashauri ya Wilaya ya Kasulu, mkoani Kigoma, imefanya hafla fupi ya kuwaaga Waheshimiwa Madiwani waliomaliza muda wao wa kuhudumu katika Baraza la Madiwani kwa kipindi cha miaka mitano, ambacho rasmi kimehitimishwa leo, Juni 20, 2025.
Hafla hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Kagoma uliopo makao makuu ya halmashauri hiyo na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo Mbunge wa Kasulu Vijijini, Mheshimiwa Agustino Vuma Olle, viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wawakilishi wa vyama rafiki, baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama pamoja na watumishi wa halmashauri.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mbunge wa Kasulu Vijijini, Mhe. Agustino Vuma Olle, amewapongeza madiwani kwa utendaji mzuri ulioepuka migogoro, hali iliyowezesha utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa ufanisi na kukamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Mhe. Eliya Kagoma, ameonyesha hisia za shukrani na heshima baada ya moja ya kumbi za mikutano ya halmashauri kupewa jina lake, akisema kuwa hilo ni tukio la kihistoria litakalobaki katika maisha yake.
“Niwaombe Waheshimiwa Madiwani tumshukuru sana Mungu, kwa kuwa wote tulioanza safari hii tupo salama hadi leo. Nawapongeza kwa kutekeleza ilani ya chama chetu kwa ufanisi mkubwa. Tumekuwa na usimamizi bora wa halmashauri na maendeleo yanaonekana dhahiri,” amesema Kagoma.
HALMASHAURI YA WILAYA YA KASULU
Anuani ya Posta: S.L.P 97
Simu ya Mezani: +255-028-2810339
Simu: +255-028-2810339
Barua Pepe: ded@kasuludc.go.tz
Copyright ©2024 kasuludc . All rights reserved.